Jumapili, 19 Julai 2015

TABIA YA MBINGUNI HAINA BUDI KUPATIKANA DUNIANI:

Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Utakatifu tu, wala si kitu kingine, ndio utakaowafanya kuwa tayari kwenda mbinguni. Unyofu na uchaji wa hakika ktk mambo ya maisha peke yake ndio uwezo wa kuwapa tabia safi, na bora, na kuwawezesha kuingia mbele za Mungu akaaye penye nuru isiyoweza kukaribiwa. Tabia ya mbinguni haina budi kupatikana hapa duniani, ama sivyo kamwe haipatikani tena. Basi, anza mara moja. Usidanganyike kuwa utafika wakati uwezapo kujitahidi kwa urahisi kuliko sasa. Kila siku huzidisha umbali wako kutoka kwa Mungu. Jitayarishe kwa ajili ya uzima wa milele. Zoeza mawazo ya moyo wako kuipenda Biblia, kupenda mikutano ya maombi, kupenda saa ya kumtafakari Mungu, na, zaidi ya yote, saa ambayo roho hushirikiana na Mungu. Uwe mwenye kufikiri mambo ya mbinguni ukipenda kuungana, na lile kundi la waimbaji wa mbinguni ktk makao ya juu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni