Jumanne, 14 Julai 2015

MASOMO YANAYOHARIBU ROHO YA MTU:

Kwa ajili ya wingi wa vitabu na magazeti vinavyomiminika daima kutoka ktk mitambo ya kuchapisha, wazee kwa vijana hufanya mazoea ya kusoma haraka-haraka na kwa juu juu tu, na hivyo ubongo hupoteza uwezo wake wa kupokea mawazo yaliyounganika na yenye nguvu. Juu ya hayo, sehemu kubwa ya magazeti na vitabu ambavyo, kama vyura wa Misri, vinatapakaa nchini, sio kwamba nivya hali ya chini tu, visivyofaa, na vyenye kudhoofisha, bali ni vichafu na vyenye kuaibisha. Matokeo yake siyo kulevya na kuharibu akili tu, bali kuchafua na kuangamiza roho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni